The House of Favourite Newspapers

Chongolo Azitaka Mamlaka za Usimamizi Miradi ya Serikali Morogoro Kuwa Makini

0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akizungumza na wananchi wa Vijiji vya Mkwajuni na Ilalo mara baada ya kujionea kero kubwa ya kukosekana kwa daraja katika mto Nguyamilinalounganisha vijiji hivyo viwili wilayani Gairo mkoa wa Morogoro.

 

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo amezitaka mamlaka za usimamizi za serikali Mkoa wa Morogoro kusimamia kwa ukamilifu miradi ya miundombinu ya serikali katika mkoa huo kwa sababu serikali imekuwa ikitoa fedha nyingi za miradi ambazo zinatokana kodi za wananchi masikini.

 

Mtoto Tefa Adua (4) akivuka Mto Nguyami ambapo kwa karibia miaka minne sasa wananchi wa kijiji cha Ilalo wamekuwa wakipata tabu baada ya daraja la awali kuharibika.

 

Chongolo ameyasema hayo akiwa katika ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya CCM Wilaya ya Gairo ambapo amepokea malalamiko kutoka kwa wananchi na Mbunge wa Jimbo la Gairo, Ahmed Shabiby kuwa madaraja matatu katika Kijiji cha Nguyami yamebomoka kwa vipindi vitatu kutokana na kujengwa chini ya kiwango.

 

Leave A Reply