The House of Favourite Newspapers

Chuchu: Hakuna Ndoa Bongo Muvi

0

MWIGIZAJI wa Bongo Muvi, Chuchu Hans amesema, ndoa za kweli hajaziona kwa mastaa hususan wanaotokea Bongo Muvi na ndiyo maana hana papara ya kuolewa.

 

Akizungumza na Risasi Jumamosi, Chuchu amesema, watu wengi ambao ni mastaa wanaokimbilia kuingia kwenye ndoa na mastaa wenzao, huwa inakuwa ni vigumu mno kutulia.

 

“Mimi kufunga ndoa mbona bado sana, maana najua ndoa za kweli bado hazijafika Bongo Muvi, bali tunaendelea kuigiza tu, zikifika ndoa za kweli, nitaguswa, lakini kwa sasa bado kabisa,” alisema Chuchu ambaye ni mzazi mwenza wa staa wa Bongo Muvi, Vincent Kigosi ‘Ray’.

Stori: Imelda Mtema

 

#LIVE: RAIS MAGUFULI AKIWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA DARAJA LA KIGONGO BUSISI

Leave A Reply