The House of Favourite Newspapers

Daktari Anaswa Akiendesha Zahanati Kimagumashi!

0
Mhusika huyo.

 

DAR ES SALAAM: Hatari! Hili ndilo neno sahihi unaloweza kuse­ma kufuatia wiki iliyo­pita, mtu mmoja aliyetambulika kuwa ni daktari, kunaswa akiwa anafanya shughuli za kuende­sha zahanati binafsi kimagu­mashi, katika eneo la Buguruni kwa Mnyamani jijini Dar es Sa­laam, kwani hakuwa na cheti wala nyaraka zozote kutoka mamlaka zinazohusika na shughuli za kitabibu

 

 

Kabati la kutunzia madawa.

 

Chanzo kilicho makini kililitonya Risasi Mchanganyiko juu ya kufanyika kwa shughuli za kitabibu kwa namna ya ujanjaujanja kwani zahanati hiyo ilikuwa ikitoa huduma kwa matatizo mbalimbali kimachalemachale.

 

Boksi la mabomba ya sindano.

 

“Sisi ni majirani hapa, lakini tumeshtushwa na utaratibu wa zahanati hii kufanya kazi ya kutoa huduma za matibabu kwa wagonjwa nyakati za usiku tu. Jambo hilo limetupa shaka tukaona hapa kutakuwa na kitu, ndipo tukaamua kuwapigia simu polisi ili waweze kuchunguza kuna nini,” kilisema chanzo hicho juu ya zahanati hiyo ambayo pia haina jina.

 

Mgonjwa akiwa kwenye zahanati hiyo.

 

Risasi Mchanganyiko lilifika eneo hilo sambamba na polisi na kushuhudia daktari huyo aliyejitambulisha kwa jina moja la Juma, akikiri kuwa yeye ni daktari wa hospitali moja wilayani Kisarawe na kukiri kuwa anatoa huduma za matibabu pasipokuwa na kibali.

 

Aina tofauti za dawa.

 

“Ni kweli jamani, najua kabisa kuwa kutoa huduma ya matibabu bila ya kuwa na leseni wala kibali chochote ni kosa, lakini nipo katika process ya kukamilisha vitu hivyo.

“Mimi ni daktari kabisa, nalijua kosa langu lakini naomba tusameheane, nitajitahidi kukamilisha taratibu za kupata leseni haraka sana,” alisema huku akiomba.

Sinki la kuoshea vifaa.

 

Kuhusu tuhuma za kufanya kazi usiku tu, daktari huyo alisema anafanya hivyo kwa kuwa muda mwingi wa mchana huwa anafanya kazi kwa muajiri wake, hivyo nafasi kwa kazi zake huwa ni muda huo pekee.

Kifaa cha kupimia.

 

Hadi Risasi Mchanganyiko linaondoka eneo la tukio, daktari huyo alikuwa bado akihojiwa na askari hao kutoka kituo kimoja cha polisi wilayani Ilala.

 

WAANDISHI WETU, RISASI MCHANGANYIKO

 

SHUHUDIA VIDEO

Leave A Reply