Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Benki ya Biashara ya DCB, Nelson Swai ametoa mada kuhusu masuala ya fedha zinazovuka mipaka Kidigitali na ujumuishi wa kifedha barani Afrika kwa baadhi ya wamiliki chipukizi wa mifumo ya Tehama wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma ya ufunguaji wa akaunti za benki za mtandaoni katika nchi mbalimbali na kufanya miamala kwa sarafu yoyote kwa makato madogo kwa kutumia proramu ya Grey ipatikanayo playstore na Appstore.