Demu Mpya wa Cristiano Ronaldo Awatoa Udenda Midume
MWANASOKA maarufu wa timu ya Real Madrid (31), ya Hispania, Cristiano Ronaldo, amepata kimwana mpya ‘mkali’ aitwaye Georgina Rodriguez ambaye vivazi vyake vinatosha kuwatoa udenda wanaume wa kila aina.
‘Mtoto’ huyo wa Kihispania alikutana na Ronaldo katika eneo maarufu la kula bata la Dolce & Gabbana ambapo mcheza kabumbu huyo alimchangamkia na kujiachia naye waziwazi katika eneo maarufu alillokwenda kujinafasi la Disneyland, jijini Paris wiki hii.
Katika kumpa kampani kimwana huyo, Ronaldo alikuwa amevaa kapelo na nywele za bandia, wakati Georgina alikuwa amejikoleza vikilombwezo vya kina aina vilivyomtoa kinoma.
Comments are closed.