Diamond Apiga Shoo Simba Day, Uwanja Wasimama (Picha+Video)
SIMBA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ Agosti 22, 2020 ametua na Helkopta na kushusha burudani ya kiwango cha juu kwa mashabiki wa Simba SC waliojitokeza.
Diamond ametoa burudani ya nguvu akiimba nyimbo mbalimbali ikiwemo ya kuisifia Simba inayoitwa Simba, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Mohammed Dewji ‘Mo’ alishindwa kujizuia na kuungana naye.
Diamond alipomaliza kupiga shoo, akaondoka eneo la tukio na usafiri aliokuja nao. Kumbuka Diamond alipiga shoo hiyo kwa takribani dakika 30, kuanzia saa 10:24 hadi 10:54 jioni, huku akiwa na madansa 68
⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx
PICHA NA RICHARD BUKOS, MUSA MATEJA, GPL