Dkt Reginald Mengi, Shigongo Watoa Heshma zao za Mwisho Kuuaga Mwili wa Ruge Mutahaba
Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Mengi, na Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Group, Eric Shigongo ni miongoni mwa waombolezaji waliotoa heshma zao za mwisho kwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, Ruge Mutahaba ambaye ameagwa leo jijini Dar es Salaam tayari kuelekea nyumbani kwao Bukoba kwa ajili ya pumziko lake la milele.
Viongozi hao walitoa heshma zao za mwisho leo katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam ambapo pia wakazi wa jiji hilo waliungana na wanafamilia katika kutoa heshma zao za mwisho.
PICHA NA RICHARD BUKOS | GPL
Comments are closed.