Ebitoke na Skendo ya Kujichubua
BAADA ya habari kuzagaa kwamba kwa sasa anatumia mkorogo (anajichubua) ndiyo maana amekuwa mweupe ghafla, mchekeshaji maarufu Bongo, Anastazia Exavery ‘Ebitoke’ ameibuka na kukanusha vikali skendo hiyo.
Akichonga na Risasi Jumamosi, Ebitoke alisema weupe wake umetokana na joto kuwa kali na katika vitu ambavyo hawezi kuvifanya ni kujichubua kwa sababu anaelewa wazi kuwa kuna madhara makubwa endapo atafanya hivyo.
“Najua madhara ya kujichubua siwezi kufanya hivyo kama watu wanavyonituhumu, nimebadilika na kuwa mweupe siku hizi tofauti na zamani kwa sababu ya joto tu na siyo vinginevyo,” alisema Ebitoke.
Stori: Memorise Richard, Dar.
Comments are closed.