Mgeni rasmi Devotha Likokola akiongea na wanawake wa vikundi mbalimbali kuwapa (hawapo pichani).
Mmoja wa wajasiriamali Ester Dalali akitoa ushuhuda kuhusu maisha yake.
Msemaji wa Kampuni ya Graca Machel akizungumza na wanawake (hawapo pichani)
Wanawake wa vikundi mbalimbali wakibadilishana mawazo na mgeni rasmi.
Likokola akikata keki.
Baadhi ya wanawake kutoka vikundi mbalimbali wakilishwa keki na Mh. Devotha Likokol.
Likokola akipokea tuzo ya mwanamke wa shoka kutoka kwa mtangazaji wa Efm radio katika kipindi cha uhondo, Dina Marios.Muda wa maakuli ukafika.Akina mama wakiserebuka na muziki wa taarab kutoka Jahaz Modern Taarab.
Katika kuelekea Siku ya Wanawake Duniani, Kituo cha Redio cha EFM kilichopo Kawe jijini Dar, jana kimevikutanisha vikundi mbalimbali vya ujasiliamali na VICOBA kutoka mkoa wa Pwani na jiji la Dar es Salaam.
Tafrija hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Litostar Park uliopo maeneo ya Salasala jijini humo ikiwa na lengo la kuwapa wanawake elimu ya ujasiliamali, kujitambua pamoja na kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili katika biashara na maisha kwa ujumla.
Aidha mgeni rasmi katika tafrija hiyo alikuwa Raisi wa VICOBA nchini, Devotha Likokola ambaye amewataka wanawake nchini kuwa wajasiriamali na wenye kuthubutu kukabiliana na changamoto zinazowakabili.