The House of Favourite Newspapers

England Yatinga Fainali ya Euro 2020, Kuvaana na Italia

0

BAADA ya Miaka 55, hatimaye Timu ya Taifa ya England imefanikiwa kuingia hatua ya Fainali ya michuano ya Euro 2020, baada ya kuifunga Denmark kwa mabao 2-1 usiku wa Jana Julai 7 kwenye Uwanja wa Wembely, Uingereza.

 

England haikuwahi kuvuka hatua ya nusu Fainali ya Michuano yoyote mikubwa Mara ya mwisho kuingia hatua hiyo ilikuwa mwaka 1966 walipoandaa kombe la Dunia, ambapo pia walifanikiwa kutwaa ubingwa huo.

 

Denmark walikuwa wa kwanza kucheka na nyavu, kupitia kwa kinda Damsgaard kwa mkwaju wa Faulo maridadi iliyomuacha mlinda mlango wa England Pickford akiwa hana la kufanya.

 

Baada ya bao hilo wajukuu wa Malkia walirudi kwa kasi na kufanikiwa kusawazisha dakika ya 39 baada ya beki Simon kujifunga akiwa katika harakati za kuokoa mpira wa kinda la Arsenal, Bukayo Saka.

 

Dakika 90 zilimalizika kukiwa hakuna mbabe na kuongezwa dakika 30, Nahodha Harry Kane aliwainua Mashabiki wengi wa Uingerza wakiongozwa na Mwana wa Malkia Prince William dakika ya 104, baada ya kufunga kwa njia ya Penati, bao ambalo limewapeka Fainali.

 

England itavaana na Italia kwenye mchezo wa Fainali utakaopigwa Jumapili Julai 11, kwenye Uwanja wa Wembely.

Leave A Reply