The House of Favourite Newspapers

ESMA AOGOPA KUAIBIKA

Esma Khan

Dada wa mkali wa Afro-Pop Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Esma Khan ameweka wazi kuwa anaogopa kuaibika kama ambavyo hutokea kwa mastaa wengi wanapotangulia mbele za haki na kukosa mahali pa kuagiwa.  Esma aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, amejifunza kwa mastaa wengi ambao walikuwa wanatamba mjini, lakini walipofariki dunia ndipo maisha yao halisi yakagundulika ikiwemo kutokuwa hata na nyumba wakati enzi za uhai huonekana wakiishi maisha ya kifahari.

“Naogopa kuaibika ndiyo maana nimenunua kiwanja maeneo ya Madale (Dar), natarajia kuanza kujenga hivi karibuni ili hata nikifa, watu wasipate shida ya mahali hata pa kuagia,” alisema Esma.

Comments are closed.