The House of Favourite Newspapers

ETI ROSA REE ANACHUKIA KUTONGOZWA

Rose Robart ‘Rose Ree’

M WANAMUZIKI wa kike ambaye anafanya vizuri kwa sasa kupitia anga la muziki wa Bongo Flava, Rose Robart ‘Rose Ree’, amefunguka kuwa hakuna kitu ambacho hakipendi kama kutongozwa.

Akichonga na Showbiz Xtra, Rosa Ree alisema kuwa mwanaume akimtongoza hujisikia vibaya na anaweza kumchukia mno, anachohitaji ni kuwa karibu na wanaume kwa ajili ya kazi na kupiga nao stori mbalimbali.

“Yaani mwanaume akinitongoza sipendi napenda kama tunakuwa marafiki tu wa muda mrefu kama ikitokea kupendana tutapendana mbele ya safari na si vinginevyo, akinitongoza mapema naona kama ananitamani tu basi alafu animwage,” alisema Rosa Ree.

Comments are closed.