Ewura: Kushuka Kwa Shilingi Dhidi Ya Dola Kumesababisha Mafuta Yapande Bei
Mamlaka ya Nishati na Maji (EWURA) imetangaza Bei Kikomo za Mafuta zinazoanza kutumika leo Agosti 2, 2023 ambapo kuna ongezeko la Bei kutokana kuadimika kwa Dola za Marekani, Mabadiliko ya Sera za Kikodi na Kupanda Bei na Gharama za Uagizaji Mafuta
DaresSalaam Petroli itauzwa Tsh. 3,199, Dizeli Tsh. 2,935 na Mafuta ya Taa Tsh. 2,668. Tanga Petroli Tsh. 3,245, Dizeli Tsh. 2,981 na Mafuta ya Taa Tsh. 2,740. Mtwara Petroli Tsh. 3,271, Dizeli Tsh. 3,008 na Mafuta ya Taa Tsh. 2,714 kwa Lita
Vipi Mdau, una maoni gani kuhusu Kushuka Thamani kwa Shilingi ya Tanzania, Bei Kubwa za Mafuta na Kuadimika kwa Dola ya Marekani Nchini?