The House of Favourite Newspapers

EWURA Yapata Tuzo Usimamizi Bora Miradi Ya Kimkakati

0

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imepokea tuzo ya mshindi wa pili katika Usimamizi Bora wa Ushirikishwaji wa Wazawa katika Miradi ya Kimkakati Nchini. TANROADS imechukua nafasi ya kwanza huku TAA ikiwa ya tatu.

Tuzo hizo zilizoandaliwa na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), zimetolewa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Mashaka Biteko wakati wa kongamano lililofanyika tar 28.04.2024; Ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, jijini Dar es Salaam.

Kongamano hilo lilishirikisha wadau mbalimbali kutoka serikalini ambao ni EWURA, PURA, TANROADS, TAKWIMU, Tume ya Madini, TIRA, Mradi wa Umeme wa Bwawa la Nyerere(JNHPP), Wizara ya Maliasili (kupitia mradi wa REGROW), PPRA, IRDP, EACOP, ERB, CRB; asasi za kiraia na taasisi za fedha.

Leave A Reply