The House of Favourite Newspapers

EWURA Yatangaza Kupanda kwa Bei ya Mafuta

0

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza ongezeko la bei ya mafuta ya Petroli na Dizeli kutokana na kuongezeka kwa bei za mafuta katika Soko la Dunia na gharama za usafirishaji.

 

Wanunuzi wa rejareja wa mafuta ya Petroli watatakiwa kuongezeka wastani wa Sh 53 zaidi kwa lita, kuongeza Sh 134 zaidi lita ya Dizeli huku watumiaji wa Mafuta ya Taa wakitakiwa kuongeza Sh 119 kwa lita ikilinganishwa na bei ya mwezi Januari.

 

Wanunuzi wa mafuta kwa jumla wataongeza Sh 52.90 kwa lita ya Petroli, Sh 133.36 kwa kila lita ya Dizeli na Sh118.31 kwa kila lita ya Mafuta ya Taa.

Leave A Reply