Fahyma Anena Bifu Lake na Lulu
WAKATI stori zikiendelea kusambaa mitandaoni amechukuliwa mumewe na mwigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’, mke wa msanii wa Bongo Fleva, Raymond Mwakyusa ‘Rayvanny’, Fahyma ‘Fayvanny’ ameanika kinachoendelea.
Tetesi za bifu la Lulu na Fayvanny ziliaza kusambaa wiki kadhaa zilizopita ikidaiwa kwamba eti walikutana saluni na kutaka kuzichapa kavukavu.
Kufuatia ishu hiyo, Shusha Pumzi ilizungumza na Fayvanny ambaye anasema kwa kifupi kuwa hahitaji kulipa jambo hilo kiki isiyokuwa ya lazima.
“Iwe ni kweli tulitaka kupigana au la, sipo tayari kuliongelea jambo hili kwa sasa kwa sababu limeshapita, nikianza kuliongelea, nitakuwa kama nazidi kulipa nafasi ya watu kuliongelea. Pia sihitaji kumuongelea sana huyo Lulu kwa kuwa hayo mambo yalishapita na sasa hivi naishi vizuri tu na mume wangu,” alisema Fayvanny.
STORI: MWANDISHI WETU
Comments are closed.