The House of Favourite Newspapers

FT: SINGIDA UNITED 4-2 YANGA, KOMBE LA SHIRIKISHO

DAKIKA 90 ZINAKAMILIKA WANAENDA KIPINDI CHA PENALTI

Dak ya 89, Pigwa hukuu Yanga wanaokoa na kupiga Counter Attack, mpira unakwenda nje

Dak ya 78, Chirwa anashindwa kumalizia vema kazi nzuri ya Tshishimbi, anaupalaza mpira unakwenda nje, goli kiki

Dak ya 75, Piga huku lakini mabeki wa Singida wanaokoa, unarudi kwa Ajib tena unambabatiza na kutoka nje

Dak ya 72, Kevin Yondan anazozana na mchezaji wa Singida, tafurani kidogo inatokea
Dak ya 71, Dante analambwa kadi ya njano, ni kadi ya kujitakia, faulo inapigwa, pigwa huku lakini mpira unaokolewa

Dak ya 57, Mhilu sasa anakwenda na mpira, penyeza kwake Ajib, anapiga krosi huku lakini inaokolewa na Kiggy Makasi
Dak ya 60, Kotinyu anang’aa zaidi eneo la kati hii leo, amekuwa mtulivu kwa dakika zote pale anapopata mpira
Dak ya 55, Singida United 1-1 Yanga

Dak ya 45, Mpira umeanz. Singida wanafanya shambulizi kali dakika hii ya kwanza kipindi cha pili, mpira unakwenda nje

DAKIKA 45 ZA KWANZA ZIMEMALIZIKA, SINGIDA 0-1 YANGA

Dak ya 44, Kutinyu anapewa kadi ya njano, ni ya kwanza katika mchezo huu
Dak ya 43, Kona inapigwa kuelekea Yanga, Kiggy Makasi anapiga lakini inatua kwa kipa Rostand

Dak ya 36, Khalfan na mpira, pasia kwake Kotinyu, gawa pembeni huku Kennedy, inapigwa moja hukuuuu, nje

Dak ya 29, Mvua inazidi kunyesha uwanjani
Dak ya 27, Hatari katika lango la Yanga, pigwa krosi kali na Kutinyu lakini mpira unavuka lango

Dak ya 25, Singida wanarusha baada ya Yanga kuutoa, unarushwa kwake Kontiyu, kwake Nizar Khalfan, piga shuti kali unagongwa kichwa unarudi dimbani
Dak ya 24, Kona inapigwa kuelekea Yanga, namna gani Singida wamekosa nafasi ya kupasia kamba, matokeo ni 0-1

Dak ya 23, Inapigwa… Gooooooooal, Yusuph Mhilu anaiandikia Yanga bao la kwanza kwa njia ya kichwa
Dak ya 21, Mpira unarushwa kuelekea Yanga, kwake Chikupe, piga mbele huku, hataari, kona, inaelekezwa Singida United

Dak ya 20, Gadiel Michael anaondolewa nje ya uwanja baada ya kuumia, mpira unaendelea
Dak ya 19, Kona, Singida wanapata kona ya kwanza, Makasi anakwenda kupiga, piga huku lakini inaokolewa

Dak ya 16, Ajiiib, piga pasi moja ya kunyanyua lakini inakosa mmaliziaji na kutua kwa Barthez kiulaiini
Dak ya 15, Jukwaa la VIP watu wanalowa na mvua inayoendelea kunyesha
Dak ya 14, Kutinyu sasa katikati mwa Uwanja, piga kwake Makasi, Makasi anampasia Mudathir Yahaya, faulo, anachezewa Nizar Khalfan

Dak ya 13, Makapu anapiga mbele kuwatafuta washambuliaji, mpira unakosa mtu, Singida wanauchukua na kuanza upya
Dak ya 12, Andrew Vincent anatolewa nje ya dimba kugangwa baada ya kuumia
Dak ya 10, Ajib anakosa nafasi ya kupachika bao, ilikuwa ni shambulio zuri kwa Yanga, mpira unaendelea
Dak ya 8, Kimvua kinanyesha uwanjani, kila timu inapambana kutafuta goli la mapema
Dak ya 6, Batambuze anaanza kati, piga pasi pembeni huku na mpira unatoka, faulo, inapigwa kwenda Yanga. Imepigwa huku mbelee, kipa Rostand anadaka kama mboga, haikuwa na madhara

Dak ya 5, Faulo imeshapigwa, inagongwa kichwa na wachezaji Singida na kurudi katikati mwa dimba, Tshishimbi anauchukua tena
Dak ya 4, Tshishimbi anachezewa madhambi, inapigwa faulo kuelekea Singida
Dak ya 3, Singida wamepata shambulizi kali la kwanza, lakini linashindwa kuzaa bao, bado 0-0
Dak ya 2, Singida wanaukokota katikati mwa Dimba, Kotinyu anapiga pasi mbele huku lakini Yanga wanaokoa
Dak ya 2, Mpira umeanza punde huku mvua ikiwa inanyesha Uwanja wa Namfua
Dak ya 1, Mpira umeanza

Comments are closed.