JPM Afanya Maamuzi Magumu kwa Mawaziri Waliotajwa Ripoti za Madini
HAFLA fupi ya Rais John Magufuli kukabidhiwa Ripoti mbili za Kamati Maalum kuchunguza biashara ya madini ya Almasi na Tanzanite nchini imefanyika Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo ripoti hizo zimekabidhiwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Yaliyojiri kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti Kamati ya Kuchunguza Almasi na Tanzanite amesema Mkataba wa Tanzanite na STAMICO hauna tija kwa nchi, ni wa kinyonyaji. Amependekeza uvunjwe.
Kati ya 1998-2017 madini ya Tanzanite yaliyopitia mfumo halali ni 5.2%. Kati ya madini ya Tsh 8Tril yaliyouzwa, serikali imepata Tsh 400B.
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
#RipotiMadini: Kuna akaunti ya wizara ya madini inapokea maduhuri ya pesa kutoka Shinyanga, tunakuomba Rais Magufuli uifuatilie. –#Zungu
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Zungu amesema ipo akaunti ya wizara ya madini inapokea maduhuri ya pesa kutoka Shinyanga, amemuomba Rais Magufuli aifuatilie kuna ubadhirifu
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
#RipotiMadini: Mwaka 2013, Tanzania ilipata hasara zaidi ya Tsh 4.5B kutokana na kinachodaiwa ni Almasi kushuka thamani baada ya kusafishwa.
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Ninashangaa kuona Wabunge kila ripoti inayoletwa wanatuhumiwa, lakini wanachi wanawachagua tu. – #SpikaNdugai
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Prof. Lipumba ameniletea wengine nimewaapisha, vyama vingine vikiona mtu hafai, nileteeni wengine wanaojali maslahi nitawaapisha-SpikaNdugai
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
#RipotiYaMadini: Nchi yetu imechezewa sana, sijui wanaotuchezea wanatuona kama binadamu au wanayama tu?
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP: Kila mmoja ajiangalie yeye na jirani yake wana maisha ya aina gani – Je haya ndo maisha tunayostahili kuwa nayo?
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Majaliwa: Kamati hizi mbili zimeundwa na vyama vyote kwa umoja. Pia wamefanya kazi kwa uhuru kamili bila kuingiliwa
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
RaisMagufuli: Tuna taarifa zote za wawekezaji walivyoshirikiana na Watanzania kuiba madini, taarifa tulifyonza kwenye mifumo yao ya kompyuta
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP: Kwenye mazungumzo walikuja watu wao 14 lakini hadi sasa wako 25. Wanaongeza majeshi maana tuna taarifa zao zote
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP: Hili suala la Tanzanite najua mna flash (mkanda) ingawa bado hamjanikabidhi. Na mimi ninayo yangu siku nyingi sana
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP: Juzi tu hapa tumekamata shehena ya Almasi ambayo imepimwa na inawezekana thamani yake ni zaidi ya ile iliyokadiriwa awali.
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @Magufuli: Aliyetupa taarifa zote hizi ni Profesa Mruma na ni yeye ametuwezesha kujua ni wapi tunaibiwa madini na kwa kiasi gani.
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP: Tuna data zote, mawasiliano yote hadi email za migodi yote. Walipogundua tunazo wakabadilisha kompyuta ‘it was too late’.
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP: Wabunge ambao wanatajwatajwa kila sehemu kwa tuhuma mbaya napendekeza vyama viandikiwe waweze kuonywa.
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP: Kuna wengine wametajwa na mimi ndio niliwateua na najua Wabunge hawa wa kwenye Kamati hawawezi kuwasingizia.
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP: Nawakabidhi vyombo vya Ulinzi na Usalama ripoti hii hapa ili waanze kuifanyia kazi.
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017
Rais @MagufuliJP : Ni heri wanichukie lakini nifanye kazi kwani tumecheza sana miaka 50. Sikuja kutafuta mchumba hapa, nimekuja kufanya kazi
— Global Publishers (@GlobalHabari) September 7, 2017