Gazeti La Ijumaa Linavyobamba Mtaani
WASOMAJI wa magazeti yanayochapwa na Kampuni ya Global Publishers wanazidi kuukubali muonekano mpya ulioboreshwa wa Gazeti la Ijumaa linalotoka kila Ijumaa.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wasomaji wa Makumbusho, Masaki, Mwananyamala, Tandale, Mabibo, Tabata, Ubungo na sehemu zingine za jiji la Dar, wamedai Gazeti la Ijumaa linazidi kuwabamba kila kukicha kutokana na kuwa na muonekano mpya wa kipekee, habari, picha na wingi wa hadithi mbalimbali.
“Nalikubali sana gazeti lenu la Ijumaa linabamba sana hata kama ulikuwa hauna mpango wa kununua, utanunua tu kwani linakuvutia kwa makala, hadithi, simulizi, na habari kibao,”alisema Yusuph Mwizagi wa msasani jijini Dar.