Gigy Money Ajifungua Mtoto Wa Kike
MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ usiku wa kuamkia leo Aprili 27, 2018 amejifungua mtoto wa kike.
Akiongea na Mtandao wa Global Publishers amethibitisha kujifungua na kusema kwa sasa amesharudi nyumbani na anamshukuru Mungu kujifungua salama.
Hata hivyo Gigy Money amesema mtoto wake haitwii Candy kama ilivyokuwa ikiripotiwa bali anaitwa Mayra.
Gigy Money ambaye kwa sasa anafanya vizuri na Ngoma ya Mimina yupo katika uhusiano wa kimnapenzi na mtangazaji wa Choice FM, Mo J.
Comments are closed.