The House of Favourite Newspapers

Dar: Jeshi la Polisi Lakamata Watuhumiwa 250

0
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar, Lucas Mkondya

 

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limewakamata zaidi ya watu 250 wanaokabiliwa na makosa mbalimbali, ikiwemo ujambazi wa kutumia silaha, unyang’anyi, uporaji, wizi wa magari na biashara ya madawa ya kulevya.

 

Katika taarifa maalum kwa waandishi wa habari iliyotolewa leo na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dar, Lucas Mkondya, Jeshi la Polisi pia limetoa ufafanuzi juu ya sakata la Halima Mdee ambapo limeeleza kwamba linamshikilia mbunge huyo wa Kawe baada ya kumkamata Ubungo Kibangu, nyumbani kwa mama yake alipokuwa amejificha baada ya kufanya kosa la kumtukana rais wa nchi, John Pombe Magufuli.

MSIKIE KAIMU KAMANDA WA POLISI DARA AKIZUNGUMZA

Leave A Reply