The House of Favourite Newspapers

Graves of The Innocents (Makaburi ya Wasio na Hatia)- 37

0

ILIPOISHIA:

Nilitazama huku na kule, nilipoona hakuna mtu anayetutazama, nilimsogelea, akanikumbatia kwa mahaba kisha akanivutia ndani. Hatukukumbuka hata kufunga mlango, kwa makusudi aliuachia ule upande wa khanga, ukadondoka chini, nikawa kama fisi aliyeona mfupa.

SASA ENDELEA…

Harakaharaka nilichojoa magwanda yangu huku nikiwa na pupa isiyo na mfano, muda mfupi baadaye tulikuwa saresare maua, nikamnyanyua Rahma juujuu na kumbwaga kwenye uwanja wa fundi seremala. Mwenyewe alionesha kufurahia sana, akanibana kwenye kifua chake kilichojaa vizuri, tukagusanisha ndimi zetu.

Hata hivyo, tofauti na mara zote ninapokuwa kwenye mazingira kama hayo, ambapo ‘Togo’ wangu huwa mkali kama nyoka koboko, nilishangaa akiwa kimya kabisa, kama hajui ni nini kilichokuwa kinataka kutokea.

Kama nilivyoeleza tangu mwanzo, sikuwa najua chochote kwenye ulimwengu wa kikubwa na Rahma ndiye aliyekuwa wa kwanza kuniingiza kwenye ulimwengu huo, akifuatiwa na Isri, tena ndani ya siku chache tu. Kwa hiyo, sikuwa mzoefu na hicho kilichotokea, kilikuwa kitu kigeni kabisa kwangu.

Nimewahi kusikia kwamba, kwa mwanaume, hakuna aibu kubwa kama kuwa na mwanamke faragha halafu ukashindwa kazi, nikajikuta nikiwa na wasiwasi mkubwa kweli ndani ya moyo wangu. Sikujua Rahma atanichukuliaje, sikujua atanidharau kwa kiasi gani, nikajikuta kijasho chembamba kikinitoka huku akili ikiwa imehama kabisa.

“Togo, vipi?” aliniuliza Rahma baada ya kubaini mabadiliko niliyokuwa nayo. Swali lake lilinifanya nizidi kujisikia aibu, nilikosa cha kujibu na kiukweli sikuwa na majibu. Alipeleka mkono bondeni yaliko makazi ya ‘Togo’ na kujaribu kumpa hamasa kwa kutumia mikono yake laini lakini ilikuwa sawa na kazi bure.

“Mshukuru sana Mungu wako, ulikuwa unaenda kumuua mtoto wa watu, mshenzi sana wewe,” nilisikia sauti ya baba ikiniongelea sikioni kwa ukali, ikafuatiwa na msonyo mrefu, nikakurupuka kwa hofu kubwa, nikawa namtazama Rahma nikiwa nimekodoa macho, kijasho chembamba kikinitoka.

Nilikumbuka tukio lililonitokea na Isri, nilipokutana naye kwa mara ya kwanza faragha, ambapo tukiwa mchezoni, ghafla ‘alikata roho’ ingawa baadaye nilikutana naye tena akiwa mzima na ndiyo yakatokea yale yaliyotokea usiku uliopita. Alichokisema baba kilinifanya nihisi kwamba huenda kuna kitu kibaya mwilini mwangu ambacho ndiyo chanzo cha yote na nikifanya masihara, kweli Rahma atakufa na kusababisha msiba mzito kwa familia yake.

Nilikumbuka pia kauli ya Isri kwamba mimi ndiye mwanaume pekee niliyeweza kuushinda mtihani wa kifo baada ya kukutana naye kimwili.

“Togo, una nini mpenzi wangu,” alisema Rahma huku akisimama, naye akionesha kushangazwa na kilichotokea. Alinisogelea na kutaka kunikumbatia lakini nilijitoa harakaharaka, nikavaa nguo zangu huku nikiendelea kuhema kwa nguvu, nikamuona Rahma akikaa pembeni ya kitanda na kujiinamia, machozi yakaanza kumtoka.

Niliondoka haraka na kuelekea bafuni, nikajifungia mlango kwa ndani na kujiinamia, nikiwa hata sielewi nini cha kufanya. Ilibidi nijimwagie tena maji, mwili wangu ukapata nguvu, nikatoka na kwenda chumbani kwangu, nikawa nimejilaza huku nikiendelea kutafakari kilichotokea.

Kwa mbali ile kiu kali ya kukutana kimwili na mwanamke ilinianza upya, nikawa najiuliza, inawezekanaje muda mfupi tu uliopita nimeshindwa kabisa kufanya chochote na Rahma na kumuacha akiwa na huzuni kubwa kwenye moyo wake, halafu dakika chache baadaye niwe na hamu kali isiyoelezeka.

Nilipokumbuka ile kauli ya baba, niliona kabisa kinachoenda kutokea ni janga kubwa kwa Rahma kwa sababu muda si mrefu, mimi ningeenda chumbani kwake au yeye angekuja kwangu, tungeanza kubembelezana na mwisho tungeishia kuangukia dhambini, na matokeo yake dhambi ingekomaa na kuzaa mauti kwa Rahma, jambo ambalo lingenifanya niishi na hatia ya kukatisha maisha ya mtu asiye na hatia milele.

Nilichokifanya, harakaharaka niliamka pale kitandani, nikavaa viatu vyangu na kutaka kutoka lakini nilikumbuka kwamba giza halikuwa limeingia kwa hiyo kutoka nje kungemaanisha kwamba ningepata madhara makubwa kama Isri alivyonipa masharti.

Niliamua kwenda kukaa sebuleni, ndugu zangu pamoja na wadogo zake Rahma wakawa wananishangaa. Kwa muda mfupi tu tuliokaa hapo nyumbani, tayari nilishaonesha tabia za ajabu sana. Kila mtu akawa ananitazama kwa macho ya chinichini, haikuwa kawaida yangu kukaa sebuleni.

Nilijikaza kiume, nikakazia macho kwenye runinga, nikawa sina habari na mtu, ukimya ukatanda pale sebuleni. Baba na baba yake Rahma walikuwa wamekaa kwenye sehemu ya kulia chakula, wakiwa wanacheza bao huku mama na mama yake Rahma wenyewe wakiwa jikoni.

Muda mfupi baadaye, Rahma alikuja na kuchungulia pale sebuleni, alipochungulia tu, macho yangu na yake yakagongana, akanionesha ishara ya kuniita kwa mkono kisha nikamsikia akitembea kuelekea chumbani kwake.

“Mungu wangu, sasa itakuwaje?” niliwaza, nikaamua kujikausha kama sijamuona Rahma, nikawa naendelea kukazia macho kwenye runinga imngawa kiukweli wala akili zangu hazikuwa pale na sikuwa najua hata kunaoneshwa nini.

Muda mfupi baadaye, Rahma alikuja tena lakini safari hii, alikuja na kukaa kwenye kochi nililokuwa nimekaa mimi, uso akiwa ameukunja. Nilijua kwamba amekasirika lakini sikuwa na namna zaidi ya kujiepusha naye, nilikuwa nampenda Rahma na sikuwa tayari kuona anapatwa na jambo lolote baya.

Alikuwa amejifunga khanga nyepesi na ndani hakuwa na kitu kabisa, nikazidi kujikuta kwenye wakati mgumu, tukawa tunatazama runinga bila mtu yeyote kumsemesha mwenzake. Hata wale ndugu zetu nadhani nao waligundua kwamba hatupo sawa kwa sababu si kawaida ya mimi na Rahma kukaa sehemu moja bila kusemeshana, tena mara nyingi tulikuwa tukicheka na kufurahi.

Dakika kadhaa baadaye, Rahma alibadili mkao aliokuwa amekaa, akanisogelea halafu akawa ni kama ameniegamia kimtindo, haikuwa rahisi kwa watu wengine kuelewa kilichokuwa kinaendelea lakini kiukweli nilijikuta nikipata msisimko mkubwa sana.

Mwisho niliamua kukata shauri maana na mimi nilikuwa nateseka, nikaamua liwalo na liwe, nikamgeukia Rahma na kumtazama usoni, naye akanigeukia, tukawa tunatazamana machoni, nikampa ishara kwamba atangulie ndani, akaniitikia huku akinitazama kwa macho yenye hisia kali za mapenzi.

Aliinuka na kutembea kwa madoido, nikawa namsindikiza kwa macho, nikawaona watu wote pale sebuleni wakitazamana. Nilishusha pumzi ndefu na kukaa vizuri kwenye kiti, nikawa navutia kasi ili na mimi niinuke na kumfuata Rahma kule ndani, tukatii kiu zetu.

“Togoo,” nilisikia sauti ya baba akiniita, nikaitika na kusimama, ilibidi nijiweke vizuri maana ilikuwa aibu kwa wote waliokuwa pale sebuleni, nikaelekea kule walikokuwa wamekaa baba na baba yake Rahma.

“Wewe sasa hivi una mambo ya kikubwa, hutakiwi kuwa unachanganyikana na wenzako, inabidi uanze kukaa na sisi baba zako, vuta kiti kaa hapa,” alisema baba, akawa ametibua shoo nzima, nilitaka kutoa visingizio lakini hakutaka kusikia chochote kutoka kwangu, ikabidi nikae na kujiinamia, wote wakawa wananitazama.

Je, nini kitafuatia? Usikose next issue.

Leave A Reply