Hazard: Messi Ndiye Mchezaji Bora Wa Dunia
STAA wa Chelsea, Eden Hazard amesema kuwa kwake yeye Lionel Messi wa Barcelona ndiye mchezaji bora wa dunia.
Kauli hiyo ya Hazard imekuja ikiwa ni wiki chache kabla ya Chelsea kukutana na Barcelona katika Ligi ya Mabingwa Ulaya, pia ikiwa inamaanisha kuwa Messi ni zaidi ya Cristiano Ronaldo wa Real Madrid ambaye ndiye mpinzani wake mkuu.
“Unapocheza soka lazima ufurahi kucheza dhidi ya wachezaji bora na timu bora. Messi ni mchezaji bora wa dunia,” alisema Hazard.
Comments are closed.