The House of Favourite Newspapers

Huseein Bashe Atoa Kauli Nzito Askofu Niwemugizi Kuhojiwa Uraia Wake

Bashe.

MBUNGE wa Nzega Mjini, Hussein Bashe ameelezwa kusikitishwa kwake baada ya Askofu wa Jimbo Katoliki la Rulenge, Wilaya ya Ngara, mkoani Kagera, Severine Niwemugizi (61), kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji kuhusiana na uraia wake.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Bashe ameandika;

I know how it feels unapo ambiwa AMA kuanza kujazishwa Fomu na kuhojiwa juu ya Uraia Wako its like kujazishwa fomu kuambiwa huyu sio Mama yako or Baba yako Pole Askofu Severine Niwemugizi wanaofanya haya hawana hata Khofu ya Mungu.

 

Askofu Niwemugizi.

Askofu Niwemugizi aliehojiwa na Idara ya Uhamiaji kuhusiana na uraia wake kwa mara ya kwanza Novemba 28 mwaka huu na mara ya pili alihojiwa Desemba 4, mwaka huu.

 

Askofu Niwemuzi aliingia kwenye headlines baada ya kueleza kuwa serikali itoe kipaumbele kwa katiba mpya ya nchi ili iweze kukamilika.

Kwa upande wake Zitto ameandika;

Askofu Aliyesema Katiba Mpya Ipewe Kibaumbele, Ahojiwa Uraia Wake

Comments are closed.