Mashabiki wa burudani usiku wa kuamkia leo walikonga nyoyo zao kwa burudani ya muziki iliyoangushwa ndani ya Ukumbi wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhiem jijini Dar ambapomakundi ya taarab ya Jahazi, Zanzibar Stars, na Ogopa Kopa yalikuwa yakishindana kutoa burudani.
Sambamba na makundi hayo pia kulikuwa na burudani ya ngoma ya ‘kibao-kata’ na msanii Dullah Makabila ambaye alipata nafasi ya kuwachombeza mashabiki waliofurika ukumbini hapo.
Burudani hiyo ilirindima ukumbini hapo mpaka majogoo huku mashabiki wakila vinono na kupiga maji.
PICHA: RICHARD BUKOS / GPL