The House of Favourite Newspapers

Jesus Ndiye Mkombozi wa Guardiola

CHAMPIONI  | Manchester, England

KOCHA wa Manches­ter City, Pep Guardiola kwa sasa ana furaha kutokana na mwenendo wa timu yake kwenye Ligi Kuu England.

City haikuwa na matokeo maz­uri kwa kipindi kirefu msimu huu na hali imekuwa mbaya sana wakati ambapo mshambuliaji wa timu hiyo, Sergio Kun Aguero, anakosekana uwanjani.

Lakini sasa anaonekana kuwa na imani kuwa timu hiyo inawe­za kufanya vizuri bila kuwa na mchezaji huyo baada ya kumsa­jili mshambuliaji raia wa Brazil, Gabriel Jesus.

Wikiendi iliyopita, City wali­ingia uwanjani na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, dhidi ya Swansea kwenye mchezo wa ligi kuu uliokuwa mkali na wa kuvutia.

Kwa mara ya kwanza, kocha wa City alimweka kwenye benchi Aguero na kumuanzisha Jesus ambaye hakika hakumuangusha kwani alionyesha kiwango cha juu sana na kuifungia timu hiyo bao safi katika dakika za mwisho na kuwapa ushindi huo ambao umewapeleka hadi nafasi ya tatu kwenye ligi.

Gabriel Jesus.

Kabla ya bao hilo, Jesus pia ndiye aliyefunga bao la kwan­za la timu yake na kuendelea kuonyesha kuwa yeye ni staa kwenye timu hiyo na Ligi Kuu England kwa ujumla.

Awali wakati anajiunga na timu hiyo hakupewa nafasi kubwa lakini kwa muda mchache tu ame­shaonyesha kuwa yeye ni mchezaji mahiri kwenye ulimwengu huu wa soka.

Wachambuzi wengi wa soka wa England wame­kuwa wakimfananisha kijana huyo na enzi za mshambuliaji hatari wa zamani wa England, Michael Owen kutokana na kasi yake na uwezo wa juu wa kupachika mabao.

Pep Guardiola

Kiwango cha mche­zaji huyo kimeanza kuonyesha kuwa kuna uwezekano mkubwa kwa Aguero akaondoka kwenye timu hiyo mwishoni mwa msimu.

Jesus kwa sasa ameshapachika ma­bao matatu kwenye michezo minne ambayo ameichezea timu hiyo ak­itokea Palmeiras ya Brazil.

City walimsajili mchezaji huyo kwa kitita cha pauni milioni 27, ambapo aliwasili kwenye timu hiyo akionekana kuwa hawezi kuwa mchezaji hatari.

“Kwangu nafikiri anawe­za kufanya vizuri zaidi ya hali ilivyo kwa sasa, kutumika chini ya michezo 10 kwenye Ligi K u u England bado hakuwezi kuku­fanya wewe ukaonekana kuwa mchezaji mahiri.

“Nimpongeze kwa kiwango anachoonyesha kwa sasa na naamini kuwa anaweza ku­tusaidia kufanya vizuri zaidi kwenye michezo mingine ijayo.

“Tulipomsajili tuliamini kuwa ni mchezaji mahiri na hili limeanza kuonekana kwenye michezo michache tu ambayo ameichezea timu hii, naamini atakuwa bora zaidi msimu ujao,” alisema kocha wa City, Pep Guardiola.

Kinda huyu mwenye umri wa miaka 19, amekuwa akita­jwa kuwa anaweza kuwa staa ajaye kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Brazil ambayo kwa sasa imekuwa ikisuasua.

Jesus ambaye alijiunga na timu hiyo kwenye usajili wa Januari, alikuwa ameshafanya mambo makubwa kwenye Ligi Kuu ya Brazil.

Hadi sasa bado siyo mche­zaji mahiri sana kwa upande wa rekodi akiwa amefanikiwa kucheza michezo 83 kwenye klabu yake ya zamani ya Palm­eras na michezo minne akiwa na City.

Takwimu zinaonyesha kuwa anaweza kuwa mchezaji hatari sana siku za usoni kutokana na wastani mzuri wa kupachika mabao kwani hadi sasa ame­shafunga mabao 31 kwenye mchezo hiyo.

Imekuwa ikiaminika kuwa anaweza kuwa staa wa timu ya Taifa ya Brazil muda mchache u j a o a k i w a a m e ­s h a i ­chezea michezo sita na ku­funga ma­bao manne.

Kumbuku­mbu kubwa al­iyonayo kwenye soka ni kutwaa me­dali ya dhahabu mwa­ka 2016 akiwa na Brazil.

 

Comments are closed.