Jiji Concert Wasanii Walivyoshindana Kuonesha Mavituz Dar Live
Ile shoo ya Jiji Concert iliyosubiriwa kwa hamu usiku wa kuamkia leo ilifanyika ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live ambapo wasanii kibao walipanda stejini kufanya yao.
Miongoni mwa waliokamua stejini ni wakali wa singeli Msagasumu, Man Fongo, Mfalme Ninja Mac Zube na wengineo.
Mambo hayakuishia hapo wapenzi wa mipasho walinogeshwa na Aisha Othaman wa Kundi la Vuvuzela Classic.
Recho Kizunguzungu naye alipanda stejini na kuonesha ukali wake kwenye Bongo Flava kwa kuwachizisha jamaa na nyimbo zake zilizoshiba mashairi ya kimahaba.
Shoo hiyo ilipigwa mpaka majogoo hivyo kuwafanya mashabiki kuruka mwanzo mwisho.
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS /GPL