RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na aliyekuwa Waziri Mkuu wake kabla ya kujiuzulu, Edward Ngoyai Lowassa wameungana na mamia ya waombolezaji na viongozi wengine wa nchi katika kuuaga mwili wa aliyekuwa mwanasiasa mkongwe nchini, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru leo jijini Dar es Salaam.
Katika tukio hilo la kuaga mwili wa mzee Kingune lililoongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaa, viongozi mbalimbali wa serikali, vyama na dini wamejitokeza kumuaga mkongwe huyo.
Mbali na Mama Samia, Lowassa na Kikwete, viongozi wengine wengine waliohudhuria ni Marais Wastaafu, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa, Mama Maria Nyerere, maalim Seif Sharif Hammad, Mama Regina Lowassa, Waziri mkuu Mstaafu, Joseph Sinde Warioba, Spika Mstaafu na Pius Msekwa.
Wengine ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Suleiman Jaffo, DC wa kinondoni, Ali Happy, majaji na viongozi wengine wa dini na taasisi mbalimbali nchini.
Mzee Kingunge alifariki dunia Februari 2 mwaka huu na anazikwa leo Jumatatu, Februari 5, katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
KUAGWA KWA ‘KINGUNGE’ KATIKA VIWANJA VYA KARIMJEE (VIDEO)
Comments are closed.