The House of Favourite Newspapers

JPM Aongoza Kikao Maalumu Baada ya Kuwaapisha Mawaziri na Manaibu

0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 09 Oktoba, 2017 amewaapisha Mawaziri 8, Naibu Mawaziri 16 na Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliowateua tarehe 07 Oktoba, 2017.

Mawaziri walioapishwa ni George Huruma Mkuchika – Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Selemani Said Jafo – Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Dkt. Charles John Tizeba – Waziri wa Kilimo, Luhaga Joelson Mpina – Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Dkt. Medard Matogoro Chananja Kalemani – Waziri wa Nishati, Anjellah Kairuki – Waziri wa Madini, Dkt. Hamis Andrea Kigwangalla – Waziri wa Maliasili na Utalii na Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe – Waziri wa Maji na Umwagiliaji.

Manaibu Waziri walioapishwa ni Joseph Sinkamba Kandege – Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, George Joseph Kakunda – Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Kangi Alphaxard Lugola – Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Stella Alex Ikupa – Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Walemavu), Dkt. Mary Machuche Mwanjelwa – Naibu Waziri wa Kilimo, Abdallah Hamis Ulega – Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhandisi Atashasta Justus Nditiye – Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Elias John Kwandikwa – Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Manaibu Waziri wengine walioapishwa ni Subira Hamis Mgalu – Naibu Waziri wa Nishati, Stanslaus Haroon Nyongo – Naibu Waziri wa Madini, Josephat Ngailonga Hasunga – Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhandisi Stella Martin Manyanya – Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, William Tate Ole Nasha – Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile – Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Juliana Daniel Shonza – Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Jumaa Hamidu Aweso – Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemuapisha Steven Nzohabonayo Kagaigai kuwa Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Pamoja na kuapishwa katika nyadhifa hizo, Mawaziri, Manaibu Waziri na Katibu wa Bunge wamekula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kilichoongozwa na Kamishna wa Maadili, Jaji Mstaafu Harold Nsekela.

Hafla ya kuapishwa kwa viongozi hao imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. George Mcheche Masaju, Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali, Wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge na Kamati za kudumu za Bunge, viongozi wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama na Viongozi wa madhehebu ya Dini na vyama vya siasa.

Mara baada ya kuapishwa Mawaziri na Manaibu Waziri wamekabidhiwa nyaraka za kazi na kuanza kazi kwa kuhudhuria Kikao Maalum cha Baraza la Mawaziri kilichoongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

09 Oktoba, 2017

===

Rais Magufuli Waapisha Mawaziri Wapya, Awapa Mwongozo

Leave A Reply