MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Damian Lubuva, amekabidhi ripoti ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 kwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam, leo.
Baada ya kupokea ripoti hiyo, Rais Magufuli amesema Sh. Bilioni 12 zilizopatikana kama chenji baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 kumalizika, zitatumika kujenga jengo jipya la Tume ya Uchaguzi mjini Dodoma.