JUX Apokelewa kwa Shangwe Global Group (Picha + Video)
MSANII wa Bongo Fleva, Juma Mussa maarufu kama (Juma Jux), leo Novemba 19, 2019 amepokelewa kwa shangwe na wafanyakazi wa Global Group alipofika kufanya mahojiano na kipindi cha Bongo 255 kinachoruka kupitia kutoka +255 Global Radio kuanzia Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa nane mchana mpaka saa kumi jioni.
Msanii huyo akiwa kwenye ofisi hizo amejionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kampuni hiyo ikiwemo suala la uandaji wa magazeti na masuala mengine ya kuhakikisha kampuni hiyo inahabarisha umma kupitia vyombo vyake ikiwemo mitandao ya kijamii.
Akiwa kwenye studi za +255 Global Radio aliweza kuzungumzia albam yake ‘The Love Album’ namna inavyofanya vizuri katika soko na kuwataka mashabiki zake kuendelea kumuunga mkono.
Comments are closed.