The House of Favourite Newspapers

Kajala Aanika Kuvunja Ndoa ya P Funk, Adai Kuishi Naye Miaka 9 – Video

MKALI wa filamu za Kibongo, Kajala Masaja ‘Kay’amefungukia madai ya kuvunja ndoa ya mzazi mwenzake ambaye pia ni prodyuza maarufu wa Bongo Records, Paul Matthyasse ‘P Funk’.

 

Akipiga Stori na global TV Online, Kajala amekanusha kuvunja ndoa ya P Funk na mkewe Samira huku akidai kuwa hayo ni mambo ya mitandaoni tu wala hayana ukweli wowote.

 

“Mimi sijavunja ndoa ya P Funk, yule ni mzazi mwenzangu, nimeishi naye miaka tisa, nimezaa naye mtoto (Paula) ambaye sasa hivi yupo kidato cha nne na ana miaka 16, si kosa mimi kupiga picha na mzazi mwenzangu,” alisema Kajala.

 

Minon’gono ya Kajala kuvunja ndoa ya P Funk na Samira iliibuka baada ya ukaribu wa wawili hao wa hivi karibuni.

MSIKIE KAJALA AKIFUNGUKA

Comments are closed.