Kala Jeremiah Alivyopata Tabu Kufuga ‘Mwembe’ Huu – Video
RAPA Kala Jeremiah ambaye hivi karibuni ameachia ngoma zake mbili #NISAMEHE na #AMERICA, amefunguka na kusema kuwa alipata wakati mgumu kubadilisha mwonekano wake ikiwemo kufuga nywele na kidevu kama ‘Osama’ ili kutengeneza uhalisia wa ujumbe aliotaka kuufikisha kwa jamii.
Amesema nyimbo hizo zina uhalisia wa maisha ya kawaida wanayokutana nayo watu wengi ikiwemo unyanyasaji wa wanawake na vijana kuamini kuwa kutoboa maisha ni kwenda Ulaya au Marekani, lakini hata hapahapa nyumbani Tanzania kuna fursa kibao ambazo wanaweza kufanya na wakatoboa.
Comments are closed.