Kanye West, Kim Kardashian Wako Ziarani Uganda
RAPA wa Marekani Kanye West (YE) na mkewe nyota wa masuala ya televisheni, Kim Kardashian West, wamewasili nchini Uganda kwa ziara binafsi yenye lengo la kupromoti utalii.
Hivi karibuni, sekta ya utalii katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki, ililaumiwa na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, kwa kutofanya juhudi za kutosha kupromoti vivutio vya asili nchini humo.
“Mastaa hao wawili walitua nchini jioni jana katika ndege binafsi,” lilisema gazeti la Watchdog Uganda la nchini humo Jumamosi iliyopita. Rapa huyo na kundi lake wameweka studio ya muziki ya muda mbugani ambako amepanga kurekodi albam mpya,” iliongeza tovuti ya gazeti hilo.
Kim Kardashian na West ambaye amebadili jina lake na kuwa YE, wanasemekana wapo mapumzikoni katika hoteli moja ya kifahari iliyoko karibu na Mto Nile kaskazini mwa nchi hiyo.
Maprodyuza wa Uganda, Swangz Avenue, wamethibitisha kuwa wanashirikiana na West katika albam yake mpya ya “Yandhi”.
Mnamo Septemba, Museveni aliitaka wizara ya utalii nchini humo na idara ya wanyamapori kuimarisha juhudi za kutangaza utalii nchini humo.
“Utangazaji wa mbuga za wanyama umekuwa ni mdogo sana. Nchi ambazo hazina cha kuonyesha katika utalii zinapata watalii wengi kuliko Uganda. Wizara ya Utalii lazima ijitahidi kutangaza utalii nchi za nje,” limesema gazeti la Kampala Post.
Credit: Aljazeera
Comments are closed.