The House of Favourite Newspapers

Kifo cha Mama Banza, Simulizi Inasikitisha

1

banza-mamaMarehemu Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’, Khadija Masanja

Imelda Mtema, Risasi

DAR ES SALAAM: Simulizi ya kifo cha mama mzazi wa mwanamuziki nyota, marehemu Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’, Khadija Masanja kilichotokea juzi Jumatatu, inasikitisha, kwa vile aliamka asubuhi ya siku hiyo akiwa mzima na ndiye aliyepokea maiti ya mjukuu wake, Sozi aliyefariki dakika chache kabla yake.

1banza1Aliyekuwa staa wa muziki wa dansi nchini, marehemu Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ (enzi za uhai wake).

Kwa mujibu wa kaka mkubwa wa marehemu Banza, Jamel alisema mpwa wake Sozi alikuja kujiuguza nyumbani kwao Sinza Kijiweni kwani alikuwa akisumbuliwa na kifua na mama yake Banza ndiye aliyekuwa akimuuguza. Siku hiyo ya Jumatatu, mpwa huyo alizidiwa hivyo wao kuamua kumpeleka hospitali ya Palestina.

Lakini kabla hawajafika hospitalini, Sozi alifariki hivyo kuwafanya warejee na mwili wake nyumbani na ni mama yao ndiye aliyewapokea na kuagiza maiti ya mjukuu wake isitiriwe vizuri chumbani.

“Baada ya muda mfupi kuna kitu tulitaka kumuuliza mama, lakini alikuwa ameenda chumbani kwake, tulipomuita na kuona kimya tukaenda chumbani kwake na kumkuta akiwa amelala na tulipojaribu kumchunguza tukagundua amefariki,” alisema Jamel.

“Yaani siwezi kuzungumza jinsi tulivyopatwa na mshtuko mkubwa sana, kwa maana tumeumia mno na hatukutarajia hicho kilichotokea kabisa baada ya kumkuta mama hapumui tena, ni maumivu makali” alisema kaka huyo huku akifuta machozi.

Mama wa mwanamuziki huyo na mjukuu wake walitarajiwa kuzikwa jana katika makaburi ya Sinza, jijini Dar.

1 Comment
  1. Jojo says

    Jamani mitihani hii mmh!

Leave A Reply