The House of Favourite Newspapers

Kikwete Akutana na Mabilionea, Aliko Dangote na Bill Gates

kiwete-dangote-na-bill-gates-2Rais Mstaafu Jakaya Kikwete (kushoto), Alhaji Aliko Dangote (katikati) na Bill Gates (kulia).

Rais wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amepata nafasi ya kukutana na mabilionea wawili wakubwa duniani akiwa ziarani Davos nchini Uswisi.

Rais Jakaya Kikwete alikutana na  tajiria namba moja Afrika, Alhaji Aliko Dangote  kutoka nchini Nigeria na tajiria namba moja duniani, Bill Gates kutoka nchini Marekani.

Viongozi hao wamekutana nchini Uswisi katika Mkutano wa Dunia wa Uchumi (World Economic Forum) wenye lengo la kujadili mustakabali na mwenendo wa uchumi wa dunia.
Mbali na masuala ya uchumi, mkutano au kongamano hilo pia hujadili kuhusu mabadiliko ya tabia ya nchi ambayo kwa sasa yamekuwa ni tishio kubwa kwa viumbe mbalimbali.

Mkutano huu huudhuriwa na viongozi kutoka mataifa mbalimbali pamoja na asasi nyingine za kuraia zikiwa na lengo la kuweka nguvu pamoja na kuifanya dunia kuwa sehemu salama ya kuishi.

Comments are closed.