Mkutano wa 11 wa Bunge la 11, Kikao cha 10, umeendelea leo Aprili 16, 2018 mjini Dodoma, ambapo asubuhi ya leo wabunge walipata fursa ya kuuliza maswali yanayohusu Wizara ya Maji na Umwagiliaji, ambapo Waziri mwenye dhamana, Mhandisi Kamwelwe na Naibu wake Jumaa Aweso, wanatoa majibu.
Baadhi ya wabunge waliopata fursa ya kuuliza maswali kwa nyakati tofauti ni Ridhiwani Kikwete wa Chalinze (CCM), Nape Nnauye wa Matama (CCM) na Joseph Haule ‘Profesa Jay’ wa Mikumi (Chadema).
Wizara nyinine zilizokuwa zikiulizwa maswali bungeni hpo ni pamoja na wizara ya Fedha na Mipango, ambapo majibu yametolewa na Naibu waziri wake Dkt. Ashatu Kijaji, na Wizara ya Elimu, iliyotolewa majibu na Naibu waziri wake William Ole Nasha.
Comments are closed.