KOCHA YANGA AIOMBEA SIMBA ITWAE UBINGWA SPORTPESA
KOCHA wa Yanga Mwinyi Zahera amesema kuwa anaomba Mungu ili timu ya Simba ifanikiwe kutwaa ubingwa wa Michuano ya SportPesa Cup.
Yanga iliondolewa jana kwenye michuano hiyo baada ya kuchapwa na Kariobang Sharks kwa mabao 3-2, leo Simba watakuwa uwanjani kucheza na FC Leopard ya Kenya.
Endapo Simba watashinda leo watakuwa wamekwenda nusu fainali ya michuano hiyo ambayo bingwa wake anachota kitita cha dola 30,000.
“Sisi tumeondolewa, naomba sana Simba ambao wanacheza kesho waweze kutwaa ubingwa huu,” alisema Zahera raia wa Congo ambaye timu yake inaongoza Ligi Kuu ya Tanzania Bara.
Comments are closed.