KRISMASI ILIVYONOGA DAR LIVE; HAKUNA ALIYELALA (Picha + Video)
WAPENZI wa burudani usiku wa kuamkia leo walishuhudia shoo ya nguvu kutoka kwa makundi mbalimbali ya burudani ambapo kundi la First Class Modern Taarab chini ya Mfalme Amigo ndilo lililofungua pazia la burudani kisha kumpisha kwa muda Mfalme wa Masauti, Christian Bella ‘Obama’, aliyekuwa na Malaika Band.
Wapenzi wa singeli nao ilikuwa siku yao ya kupasha misuli baada ya Vairas Mdudu kuvamia jukwaa na kisha kumuachia jukwaa Yuda Msaliti ambaye baada ya kuwapeleka ‘mpesempese’ mashabiki wa burudani na aliwapisha tena First Class ambao walifunga shoo muda wa kufungulia kuku.
Mchanganyiko huo wa burudani ulionekana kumfanya kila mtu akate kiu yake ya burudani.
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.