Kuelekea Tamasha La Tuzo Za Filamu Kesho Jumamosi, Mastaa Na Wadau Wafanya Kongamano
Dar es Salaam 15 Desemba 2023: Bodi ya filamu nchini katika kuelekea kwenye Tamasha la Tuzo za filamu nchini kesho Jumamosi, imefanya kongamano na wadau wa filamu na kujadili maslahi ya kazi hiyo.
Katika kongamano hilo wasanii na wazalishaji wa filamu walitoa mapendekezo kwa bodi hiyo kama serikali ikayapokea na kuwaahidi kuyafikisha serikali kuu kwa ajili ya kuyafanyia kazi.
Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika Ukumbi wa Super Dome uliopo Masaki jijini Dar ambapo mastaa wa filamu karibu wote wanatarajiwa kuhudhuria.
Kwa upande wa Serikali Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Dk. Kiagho Kilonzo na maofisa wa bodi hiyo ndiyo walioiwakilisha serikali kujibu hoja za wadau wa filamu waliofurika kwenye kongamano hilo. HABARI/PICHA NA RICHARD BUKOS WA GLOBAL TV