The House of Favourite Newspapers

Kwenye ‘Mpunga’ Trump si Mtu wa Mchezo Mchezo!

483208412-real-estate-tycoon-donald-trump-flashes-the-thumbs-up-jpg-crop-promo-xlarge2

Mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya Republican, Donald John Trump.

trumpjet-1 trumpjet-2

 Ndege ya Donald Trump  Boeing 757, yenye thamani ya dola millioni 100.

donald-trump-planeTrump baada ya kushuka katika ndege yake  katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa San Jose.

donald_trump_gettyimages-150512783_sy9248h Trump akiwa ofisini kwake katika jengo la  Trump Tower, Manhattan.trump-las-vegas

 Jengo la Trump Hotel Las Vegas

Trump Ocean Club International Hotel and Tower

Trump Ocean Club International Hotel, ipo katika Jiji la Panama.

1414631359467860518

Trump International Beach Resort

7ab2203b9c2d418a4453e0cea54c50f7Trump Ocean Club International Hotel.

trump_international_hotel_tower_a191108_2

Trump International Hotel & Tower Dubai

trump_tower_7181836700_nt8byqTrump Tower, Manhattan.

palm-trump-international-hotel-and-towerDonald Trump Tower amewekeza dola milioni 400, Dubai.

ct-no-trump-signs-in-chicago-met-0428-20160428

DONALD TRUMP JOHN alizaliwa 14 Juni 1946 huko Jamaica Estates, Queens akiwa ni mtoto wa pili kwenye familia ya watoto wanne wa familia ya Mary na Fred Trump na kukulia katika Jiji la New York, Marekani.

Upande wa baba yake (Fred Trump aliyefariki mwaka 1981), alikuwa mzaliwa wa Ujerumani na mama yake (Mary) ni mzaliwa wa Scottish.

Trump alianza kusoma katika Chuo Kikuu cha Fordham kilichopo Bronx mwaka 1964, miaka miwili baadaye alihamishiwa katika Shule ya mambo ya fedha na Uchumi ya Wharton iliyopo Chuo Kikuu cha Pennsylvania  ambako alihitimu shahada ya kwanza katika masuala ya uchumi mwaka 1968 kabla ya kujiunga na kufanya kazi kwenye kampuni ya familia yake iliyoitwa Elizabeth Trump & Son.

Mwaka 1971 Trump alikabidhiwa kuongoza makampuni na biashara za baba yake ambapo alipata mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi ambayo mpaka sasa ndiye mkurugenzi wake mkuu.

Trump ambaye ni baba wa watoto watano, ni mfanyabiashara mkubwa na bilionea nchini Marekani, pia ni mtayarishaji wa vipindi vya televisheni.

Baadhi ya mali anazomiliki

Trump Ocean Club International Hotel and Tower lililopo Panama City, Panama

Trump Tower lililopo Manhattan

Wollman Rink lililoko Central Park

Trump Taj Mahal lililoko Atlantic City, New Jersey

Turnberry Hotel, iliyoko Ayrshire, Scotland

Trump Hotel Las Vegas

Trump International Hotel & Tower ya New York

Trump International Hotel & Tower ya Chicago

Trump International Hotel ya Las Vegas

Trump International Hotel ya Waikiki Beach Walk

 Trump SoHo ya New York

Trump International Hotel & Tower ya Toronto

Taasisi ya Donald J. Trump

Branding na licensing

Ndege kubwa ya Trump’s Boeing 757, maarufu kama “Trump Force One”.

Utajiri

Mwaka huu (2016), Jarida maarufu la Forbes lilikadiria utajiri wa mali za Trump kuwa unafikia dola bilioni 3.7. Ameweka rekodi ya kuwa mwanasiasa mwenye utajiri mkubwa zaidi kwenye historia ya nchi hiyo.

Ikijumulishwa na thamani ya kampuni yake (brand), Trump anakadiliwa kuwa na utajiri sasa wa dola bilioni 10 na kuwa tajiri namba 324 wa dunia na wa 156 kwa nchi ya Marekani.

Trump ni Mwenyekiti na Rais wa Shirika Kibiashara la Trump (Trump Organization) lenye makao yake makuu katikati ya Mji wa Manhattan ambalo linamiliki majengo mengi marefu, hoteli, kasino,  timu za gofu, ndege na miradi mbalimbali mikubwa ya maendeleo nchini Marekani na nje ya Marekani.

Ni mwanasiasa wa Chama cha Republican na anagombea urais wa Marekani kupitia chama hicho mwaka huu, uchaguzi utaofanyika Novemba 8.

Comments are closed.