Lewandowski Aomba Kusepa Bayern Munich
MSHAMBULIAJI wa timu ya Taifa ya Poland, Robert Lewandowski ameomba kuondoka katika Klabu yake ya FC Bayern Munich ya nchini Ujerumani.
Lewandowski ambaye bado ana mkataba na mabingwa hao wa Bundesliga hadi mwaka 2021, amemkodi Wakala Pini Zahavi amsaidie kufanya mazuyngumzo ili Klabu hiyo imuachie. Zahavi ni wakala aliye nyuma ya mafanikio ya Neymar na dili lake la kwenda PSG,
Kwa misimu kadhaa sasa, Lewandowski amekuwa akihusishwa na kujiunga na Real Madrid, na sasa wakala wake Pini Zahavi amethibitisha kwamba ni kweli mteja wake anataka kuondoka Allianz Arena. Chelsea, PSG ni vilabu vingine ambavyo vinahusishwa na uhitaji wa saini ya Robert.
Comments are closed.