The House of Favourite Newspapers

Lil Nas X Na Cardi B Wameshitakiwa Kwa Kuiba Wimbo

Lil Nas X na Cardi B wameshitakiwa na prodyuza Brandon Lee, ambaye anasema wimbo wao ‘Rodeo’ ni mfano wa kazi yake.

Lee amesema aliandika wimbo huo ambao uliachiwa kwa jina la Broad Day, lakini kitu cha ajabu alikuja kuusikia kwa wawili hao wakiwa wameutumia bila kumpa heshima ya anachostahili.


Rodeo ni wimbo unaopatikana kwenye 7, EP ya Lil Naas X ambayo ina nyimbo saba ukiwemo ‘Old Town Road’ ambao umemuweka mwanamuziki huyo kwenye nafasi nzuri.

Wakati prodyuza Lee amefikisha kesi yake mahakamani, muimbaji mwingine Fiona Apple amesema Lil Nas X hakumuomba ruhusa ya ku-sample mmoja kati ya nyimbo zake.

Comments are closed.