The House of Favourite Newspapers

Mambosasa: Vigodoro Haviendani na Ustaarabu wa Dar- VIDEO

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amewaomba wadau mbalimbali wa amani kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi ili kuendeleza hali ya usalama iliyopo sasa katika Jiji la Dar es Salaam.

 

“Wazazi katika kipindi hiki cha sikukuu kila mmoja atimize wajibu wake wa kuhakikisha anajilinda yeye mwenye na watoto wake kwa kufanya hivyo sikukuu hii haitakuwa na madhara kwao, katika sikukuu hii hatutarajii kuona Disco Toto, kwani mpaka sasa hatujapokea taarifa yoyote ya kuomba kibali hicho, kwahiyo Disco Toto ni marufuku katika Jiji la Dar es Salaam na tunataka watu washerehekee maeneo yenye utulivu na salama zaidi kwao.

“Ngoma za vigodoro haziendani na ustaarabu wa Dar es Salaam na niseme tu kwamba tutakushugulikia kabla hata haujaanza kucheza ngoma hiyo”.

Lazoro Mambisasa – Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam amepiga marufuku kusherekea sikukuu za mwisho wa mwaka kwa kulipua fataki pasipo kuwa na kibali cha kutumia fataki hizo kwenye maeneo maalumu.

 

Comments are closed.