The House of Favourite Newspapers

Mkutano wa Viongozi wa Dini na Waziri Mwakyembe!

0

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Harrison Mwakyembe amesema Serikali inatambua haki ya vyombo vya habari katika kukosoa, kujadili na kuchambua masuala mbalimbali.

Hata hivyo, amesema visivuke mipaka na kuhatarisha masilahi ya Taifa katika kufanya kazi zake.

Dk Mwakyembe amesema hayo leo Jumatano Oktoba 25,2017 ikiwa ni siku moja baada ya Serikali kulifungia gazeti la Tanzania Daima.

Amesema hayo katika mkutano na viongozi wa madhehebu ya dini uliojadili masuala ya amani na uzalendo kuelekea uchumi wa viwanda.

Dk Mwakyembe amesema Serikali inatambua uhuru wa vyombo vya habari lakini amewataka wamiliki wake na waandishi kwa jumla kufahamu sheria na vifungu vya Katiba ili kulinda masilahi ya Taifa katika utoaji wa taarifa.

Amesema ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatoa haki ya uhuru wa mawazo lakini ibara ya 30 inaweka mipaka kwa haki na uhuru huo.

Waziri Mwakyembe amesema katika kufikia uchumi wa viwanda vyombo vya habari ni vya muhimu ili kufikisha taarifa.

Amewataka waandishi wa habari kuzingatia weledi ili Taifa liendelee katika sekta mbalimbali na kufikia uchumi wa kati.

Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum amesema Watanzania wanatakiwa kuwa wazalendo kwa kuipenda nchi yao na kukemea mambo yote ambayo yanahatarisha amani.

“Wasomi na viongozi ni wakati wao wa kukemea mambo maovu ikiwemo rushwa na ufisadi kwa kuwa kufanya hivyo ni njia mojawapo ya kuipenda nchi na kulinda amani,” amesema.

Leave A Reply