The House of Favourite Newspapers

Majaliwa Azungumza Katika Swala na Baraza la Eid Dar -Video

0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Baraza la Eid El Adh’haa lililofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam, Julai 31, 2020.

Eid Al Adha Jijini Dar es Salaam, Majaliwa amesema kuwa ni muhimu kwa wanasiasa kueleza yale waliyopanga kuwasaidia wananchi kuliko kubeza yale yaliyofanywa na wengine na kukashfu.

 

“Tujiepushe na lugha za uchochezi, tujiepushe na lugha za bezo, tujiepushe na lugha za kashfa kazungumze kile ambacho utawatendea wananchi,” amesema Majaliwa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akishiriki katika Swala ya Eid El-Adh’haa iliyofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam, Julai 31, 2020. Wa tatu kushoto ni Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally , Sheikh Mkuu na Mufti wa Tanzania na wa tano kushoto ni Sheikh Alhad Salum, Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam.

Waziri Mkuu pia amewashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuimarisha amani na mshikamano nchini kwa kutoa mawaidha mazuri yenye lengo la kujenga jambo ambalo limekuwa msaada mkubwa kwa Taifa.

 

Akielezea kuhusu hayati Benjamini Mkapa ,amesema kuwa waislamu watamkumbuka kwa kuanzisha Chuo Kikuu cha waislamu kwa kutoa majengo ya Serikali na kukabidhi kwa waislamu na hivyo kuanzishwa kwa Chuo Kikuu hicho kilichopo mjini Morogoro.

Waumini wa Dini ya Kiislamu wakiswali swala ya Eid El Adh’haa kitaifa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam, Julai 31, 2020.
Waumini wa Dini ya Kiislamu wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipozungumza katika Swala na Baraza la Eid El Adh’haa kitaifa kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam, Julai 31, 2020.

 

⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP:

⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8

Leave A Reply