The House of Favourite Newspapers

Lulu Diva: Nitakuwa Smati Hata Kama Nauguza!

0

SEX lady kunako gemu ya muziki wa Bongo Fleva Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ amesema kuwa ni kweli mama yake anaumwa lakini hiyo haimfanyi yeye kutojiweka vizuri.

Akizungumza na RISASI VIBES hivi karibuni, Lulu Diva alisema kuwa kuna baadhi ya watu wanataka awe mchafu eti kwa sababu tu mama yake yupo nyumbani ni mgonjwa jambo ambalo sio sawa.

“Kitu ambacho watu wengi hawakijui ni kwamba mimi natafuta pesa kwa ajili ya mama yangu, ili aweze kutibiwa vizuri, kula vizuri na kuishi sehemu nzuri, natamani siku moja mama yangu aweze kukaa na kuzungumza chochote na mimi kwa sababu sasa hivi ni mtu wa kukaa tu nyumbani, lakini hiyo hainizuii mimi kutovaa vizuri,” alisemaLulu Diva.

Stori na Memorise Richard

⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx

Leave A Reply