The House of Favourite Newspapers

MAAJABU: OPRAH ANA MIKONO MITATU, MWIGIZAJI MIGUU MITATU!

Mtangazaji na mmiliki maarufu wa vipindi vya televisheni, Oprah Winfrey, 63, (kushoto) anaonekana  ana mikono mitatu katika picha akiwa na mwigizaji  Reese Witherspoon  na Tom Hanks waliyopigwa kwa ajili ya jarida la Vanity Fair katika toleo la  24 la kila mwaka la ‘Hollywood’.  Mkono wake wa kwanza ni ulioshika kiuno chake, wa pili uko juu ya paja lake na wa tatu ukiwa umeshika kiuno cha Reese kupitia kwa nyuma!

Pamoja na kumwonyesha Oprah akiwa na mikono miwili ya kawaida, hapa kuna kosa likimwonyesha Reese akiwa na miguu mitatu —  miguu miwili iliyo kulia na mguu wa tatu unaotokea juu kwenye sketi yake ndefu iliyochanwa pembeni na kuendelea hadi chini pembeni mwa  miguu hiyo miwili!

JARIDA maarufu nchini Marekani la Vanity Fair linalobeba habari za utamaduni, fasheni na matukio ya sasa na kuchapishwa na kampuni ya Condé Nast, hivi karibuni lilifanya kioja katika kuhariri picha zake kwa ajili ya toleo la 24 la mwaka la ‘Hollywood’ ambapo katika picha ya kwenye jalada lake, mtangazaji maalum wa vipindi vya televisheni, Oprah Winfrey (63), alijikuta akiwa na mikono mitatu, na mcheza sinema Reese Witherspoon (41) alionekana ana miguu mitatu!

Hii ni picha iliyotakiwa kuwa orijino lakini ikafanyiwa marekebisho baada ya kuondolewa kwa James Franco. Katika jalada hilo jipya kuna mastaa (kutoka kushoto kwenda kulia): Nicole Kidman, Tom Hanks, Michael B. Jordan, Zendaya, Jessica Chastain Claire Foy, Michael Shannon, Harrison Ford, Gal Gadot, Mhariri wa Vanity Fair, Graydon Carter  na Robert De Niro. 

Katika picha hiyo, Oprah anaonekana ana mkono mmoja ulioshikakiuno chake, mmoja ukiwa juu ya paja lake na mwingine umezingira kiuno cha Reese.  Naye Reese aliye kando ya Oprah, pamoja na kuwa na miguu mwili inayoonekana mbele, anaonekana ana mguu wa tatu unaotokea juu kwenye sketi yake ndefu iliyochanwa pembeni na kuendelea hadi chini pembeni mwa  miguu hiyo miwili!

Mwigizaji Reese Witherspoon akiwa katika picha yake binafsi akimsindikiza mwanaye kwenda shule.

Watu waliuvamia mtandao wa Twitter siku ya Alhamisi na kulikejeli jarida hilo kwa makosa hayo ambapo ilijulikana kwamba kasoro hizo zilitokana na kuondolewa kwa picha ya James Franco kwenye picha hiyo kutokana na madai ya tabia yake mbaya kuhusiana na masuala ya ngono.

(WALUSANGA NDAKI/MITANDAO/MASHIRIKA YA HABARI)

Comments are closed.