Maandalizi Ya Tigo Fiesta 2017, Viwanja Vya Leaders Club Yalivyokuwa
Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, alisema kwamba shoo ya leo itakuwa na utofauti mkubwa dhidi ya zile zilizopita kwani wasanii wamejiandaa vizuri kutoa shoo baab’kubwa pia kutakuwa na sapraiz ambayo anaamini itawafurahisha mashabiki watakaojitokeza Leaders.
Ruge alisema licha ya kuwa shoo ya aina yake pia wasanii kabla ya kuanza kufanya makamuzi yao watapata fursa ya kutambulishwa kila mmoja kwa mashabiki kwa mtindo wa kupita jukwaani kisha kwenda kukaa nyuma ya jukwaa kusubiria muda wake wa kukamua.