The House of Favourite Newspapers

Magufuli ateua Makamu Mwenyekiti Bodi ya TCAA

0
magufuli_0
Rais Magufuli (aliyekaa) akiwa na baadhi ya watendaji wa Ikulu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Longinus Kyaruzi Rutasitara kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA).
Prof. Longinus Kyaruzi Rutasitara anachukuwa nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Nyamajeje Calleb Weggoro ambaye muda wake umemalizika.
Uteuzi huu umeanza tarehe 16 Julai, 2016.
Kwa mujibu wa sheria ya Mamlaka ya usafiri wa anga ya mwaka 1977 Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo huteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo Mwenyekiti akitoka Tanzania Bara, Makamu Mwenyekiti hutoka Tanzania Zanzibar na kinyume chake.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amempandisha cheo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Kedmon Andrew Mnubi kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP).
SACP Kedmon Andrew Mnubi pamoja na makamishna wengine 59 ambao Rais Magufuli amewapandisha vyeo kuanzia tarehe 16 Julai, 2016 watakula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kesho jumatatu tarehe 18 Julai, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam saa tatu asubuhi.
Rais Magufuli atakuwepo wakati Makamishna wote 60 wakila kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma, zoezi ambalo litaendeshwa na Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Salome Kaganda.
Wote wakaohudhuria tukio hili wanatakiwa kufika Ikulu kabla ya saa mbili na nusu asubuhi na wataingia kupitia lango kuu la mashariki (lango la baharini).
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
17 Julai, 2016
Leave A Reply